Jumatano, 12 Oktoba 2016

Jinsi ya kukata nyama za tumboni kwa wewe mwenye kitambi-kwa mwanaume

1.Acha kula chakula chochote chenye jamii ya sukari kwa muda wa wiki 10. 

2. Fanya mazoezi kabla hujala kitu chochote mwilini. Dakika ishirini zinatosha. Utachoma mafuta mengi zaidi tofauti na ukifanya mazoezi baada kula.

3. Beba vyuma. Hayo ndio mazoezi yatakayokusaidia kutimiza hilo lengo ndani ya wiki kumi. Kukimbia ni mazoezi ya wanawake.

4. Vyakula vyako vitakuwa ni jamii ya protini na mafuta. Mfano-nyama nyekundu[sio mchuzi wa nyama], mayai ya kuchemshwa,maparachichi,korosho,karanga,kuku(sio wa kukaanga),samaki...............

Najua wengi wenu wa mnaofanya kazi maofisni mnapenda kula mananasi,maembe,matikiti,machungwa,chapati,maandazi,chipsi,chipsi mayai,Pepsi cola, Coca cola,juisi ya matunda iliyojaa sukari,ceres,debonairs,vitumbua n.k..

Watu mnasema mafuta yananenepesha. Kwamba eti binadamu asile nyama nyekundu, au nyama ya aina yeyote ile. Mwili wa binadamu haujatengenezwa kutunza mafuta mwilini. Sema huo mwili wako na wangu unapenda kutunza sukari. Sukari ndio inayotunza mafuta. 

Kwahiyo,kwa mfano,kama unakula kitimoto na kushushia na safari moja baridi,elewa kwamba kitambi chako kinatokana na sukari iliyomo kwenye bia. Hiyo sukari ndio itakayotunza hayo mafuta ya kitimoto kwa kiwango kikubwa katika mwili wako. Nimefuata hii protocol kwa muda zaidi ya wiki kumi. Nakuahidi ya kwamba,ukiacha kula sukari ,HAITAWEZAKANA kwa mwili wako kutunza mafuta yaliyopo kwenye ki-pipa chako. Hayo mafuta yatashuka tu. 

Kwa msaada zaidi nenda:Getalife.com. Ingia kwenye section ya nutrition na soma kila kitu humo ikiwemo hii post- fat loss diet 101. Huu ndio ushauri nilioufuata mimi na umenisaidia.

0 maoni:

Chapisha Maoni