Jumatano, 12 Oktoba 2016

USHAURI WA BURE KWA MWANAMKE TEGEMEZI

Katika   harakati za kupambana na umaskini ,wanawake  wengi  wamekuwa wakihangaika huku na kule kutafuta kipato ambacho kinaweza kuzitunza
familia zao.

Katika harakatri hizo wapo ambao wameweza kufikia malengo yao  na wapo ambao  wamekata tamaaa kutokana na ugumu washughuli ambazo wao binafsi
wamezichagua  na baadala ya kuwaletea mafanikio zimekuwa zikiwaletea hasara.black-group-of-female-friends-pf

Hata hivyo  bado wapo wanawake wengi  ambao wamekuwa tegemezi kutokana na kushindwa kujishuhulishja na shuhuli ndogo ndogo ambazo
zingeweza kuwaingizia  kipato kwa namna moja ama nyingine na kuweza kuyamudu mahitaji yao.

Wengi wamekuwa wakijiweka  nyuma  wakiamini kwamba  mwanaume ndiye mwenye wajibu wa kuitunza familia, Hali hiyo imekua ikisababisha wanawake  wengi kushindwa kufanya mambo mbalimbali ya maendeleo kutokana na kile wanachoachiwa  kuwa kidogo ambacho hakitoshelezi.

Baadhi ya  wanawake  wamekua na tabia ya  kukaa bila kujishuhulisha na kushindwa hata yale mahitaji ambayo wangeweza  kuyatatua wakishindwa na matokeo yake  kubaki kuilaumu serikali  kuwa  haitimizi
wajibu wake.

Wengine  wamekua  wakikaa kibarazani  na kupiga soga ambazo  zimekuwa zikiwagombanisha hasa kwa wale ambao wanakuwa wanang’ata na kupuliza ,hawa ni wale watu ambao anachukua maneno huku na  kuyapeleka  kule na mwishowe kusababisha  ugombanishi, Ushauri wa bure kwa wanawake wa namna hii ni vyema wakajihusisha na masuala ya ujasiriamali kwa ujasiriamali umewasaidia wengi na kuwanufaisha.

0 maoni:

Chapisha Maoni